Young Kacha - Bora baba angekuwa mbunge lyrics

Published

0 178 0

Young Kacha - Bora baba angekuwa mbunge lyrics

Intro:ts all about hustle....hustle all day...... Verc:1 MikSa kuku mikSa bata zinawafanya wawe stebo/ Kila siku mi tembele japo muhimu vegetable/ Mpaka wana kinai utamu kama samaki kupiga mbizi/ Mie vinono na vitamu naishia kuviota kwenye njozi/ Yule baba ake mbunge, wangu mwananchi wa kawaida/ Baba angekuwa mbunge nisingezijua shida/ Wanajenga barabara ilimradi kwa faida yao/ Ili wakija kwenye kampein wasiumize magari yao/ Wakiondoka ndo wameondoka wanatuachia vumbi tu/ Hafueni kwa wakishua sio kayumba wa miguu/ Kiatu cha shule miaka mitatu, uku wa mbunge ye anachange/ Skonga hupelekwa na gari, mi mpaka soli husema please/ Elimu yangu yakikayumba nasoma kwa mwanga wa jirani/ Uku wa mbunge ye ana happy na tayari yupo mamtoni/ Bora baba angekuwa mbunge dodoma bungeni/ Labda izi shida ningeishia kuziota ndotoni...... Chorus: Life is hard matatizo yamepangana/ Hakuna kazi kwa ofisi wanabebana/ Life chungu sio sweet kama banana/ Stress nyingi kwa kichwa zinagandana.....